Thursday 19 September 2013

NICKI MINAJ APATA TUHUMA ZA KUCOPY NYIMBO YA "STARSHIP"


Rapa Nicki Minaj, ameshitakiwa kwa kosa la ‘kucopy na kupest’, kwa mujibu wa tuhuma hizo singo ya Nicki ya Starship iliyofanya vizuri mwaka 2012, alicopy kutoka kwenye kibao cha Neu Chicago kilichofanya na msanii chipukizi mmoja anayejulikana kwa jina la Clive Tanaka.
Kwa mujibu wa gazeti la Chicago Tribune, Clive amemshitaki msanii huyo kwa kuiba sehemu ya mistari yake iliyopo kwenye kibao cha Neu Chicago na kukitumia katika singo yake hiyo iliyotamba mwaka huo.
Kesi hiyo ilifunguliwa Jumanne septemba 10 mwaka huu, kwenye Mahakama ya wilaya Chicago pia imewataja Mtayarishaji RedOne, waandishi wa wimbo wa Starship kuwa nao pia walihusika katika kwenye kuiba wimbo wake