Tuesday 30 July 2013

Shilole amkumbuka Marehemu Sharo Milionea kwa staili hii.

Leo kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii, mwigizaji na mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya zuwena
Mohamedi ama Shilole ameonesha hisia zake kwa namna anavyomkumbuka marehemu Hussein Ramadhan kipindi hiki cha mfungo wa mwezi wa Ramadhani.
Kupitia ukurasa huo Shilole ameandika…
“Ilikuwa ramadhan kama ya leo tulienda kwenye interview kwa dina wote. Tulifanya mengi sote leo nipo mwenyew nakumis sana. Mwenyez mungu akupunguzie adhabu ya kabri amen”
Marehemu Sharo Milionea alifariki dunia mwezi wa kumi na moja mwaka jana kwa ajali ya gari huko mkoani Tanga.
RIP Sharo Milionea